Isaiah 3:1-6
Hukumu Juu Ya Yerusalemu Na Yuda.
1 aTazama sasa, Bwana,
Bwana Mwenye Nguvu Zote,
yu karibu kuwaondolea Yerusalemu na Yuda
upatikanaji wa mahitaji na misaada,
upatikanaji wote wa chakula na tegemeo lote la maji,
2 bshujaa na mtu wa vita,
mwamuzi na nabii,
mwaguzi na mzee,
3 cjemadari wa kikosi cha watu hamsini
na mtu mwenye cheo, mshauri,
fundi stadi na mlozi mjanja.
4 dNitawafanya wavulana wawe maafisa wao,
watoto ndio watakaowatawala.
5 eWatu wataoneana wao kwa wao:
mtu dhidi ya mtu, na jirani dhidi ya jirani yake.
Kijana atainuka dhidi ya mzee,
mtu mnyonge dhidi ya mtu mwenye heshima.
6 Mtu atamkamata mmoja wa ndugu zake
katika nyumba ya baba yake na kusema,
“Unalo joho, sasa uwe kiongozi wetu,
tawala lundo hili la magofu!”
Copyright information for
SwhKC