Isaiah 3:1-6

Hukumu Juu Ya Yerusalemu Na Yuda.


1 aTazama sasa, Bwana,
Bwana Mwenye Nguvu Zote,
yu karibu kuwaondolea Yerusalemu na Yuda
upatikanaji wa mahitaji na misaada,
upatikanaji wote wa chakula na tegemeo lote la maji,

2 bshujaa na mtu wa vita,
mwamuzi na nabii,
mwaguzi na mzee,

3 cjemadari wa kikosi cha watu hamsini
na mtu mwenye cheo, mshauri,
fundi stadi na mlozi mjanja.


4 dNitawafanya wavulana wawe maafisa wao,
watoto ndio watakaowatawala.

5 eWatu wataoneana wao kwa wao:
mtu dhidi ya mtu, na jirani dhidi ya jirani yake.
Kijana atainuka dhidi ya mzee,
mtu mnyonge dhidi ya mtu mwenye heshima.


6 Mtu atamkamata mmoja wa ndugu zake
katika nyumba ya baba yake na kusema,
“Unalo joho, sasa uwe kiongozi wetu,
tawala lundo hili la magofu!”
Copyright information for SwhKC